Deus Mndeme- Poster Master |
Tanzania
imeungana na nchi nyingine za Afrika katika kuadhimisha siku ya posta barani
Afrika
Akizungumza
katika maadhimisho hayo yaliyofanyika jijini Dar es salaam,Posta Masta Mkuu
Deus Mndeme amesema shirika la posta nchini linaadhimisha siku hiyo huku
likijivunia ufanisi katika mipango yake mbalimbali
Ametaja mafanikio
hayo kuwa ni pamoja na kupanuliwa na kuimarishwa kwa mtandao wa kutuma na
kulipia fedha,kuimarishwa kwa usambazaji wa teknolojia mpya kwa ajili ya
kuboresha huduma za intanet.
Amesema
shirika hilo kwa hivi sasa limeanza kutumia mfumo wa kisasa wa intanet
unaomwezesha mteja kufuatilia taarifa za barua au kifurushi alichotuma
Posta masta
huyo mkuu ameongeza kuwa shirika hilo linashirikiana na mamlak aya mawasiliano
nchini TCRA katika kubuni na kuweka
mikakati ya utekelezaji wa mfumo wa anwani za makazi na postikodi
Katika hatua
nyingine bwana Mndeme amesema hivi sasa shirika lake linataka kujiendesha
kisasa zaidi ili kuzidi kuwashawishi vijana watumie huduma zao.
No comments:
Post a Comment