Karibu katika blog yetu

Friday, January 18, 2013

SIKU YA POSTA AFRIKA


Deus Mndeme- Poster Master




Tanzania imeungana na nchi nyingine za Afrika katika kuadhimisha siku ya posta barani Afrika

Akizungumza katika maadhimisho hayo yaliyofanyika jijini Dar es salaam,Posta Masta Mkuu Deus Mndeme amesema shirika la posta nchini linaadhimisha siku hiyo huku likijivunia ufanisi katika mipango yake mbalimbali

Ametaja mafanikio hayo kuwa ni pamoja na kupanuliwa na kuimarishwa kwa mtandao wa kutuma na kulipia fedha,kuimarishwa kwa usambazaji wa teknolojia mpya kwa ajili ya kuboresha huduma za intanet.

Amesema shirika hilo kwa hivi sasa limeanza kutumia mfumo wa kisasa wa intanet unaomwezesha mteja kufuatilia taarifa za barua au kifurushi  alichotuma

Posta masta huyo mkuu ameongeza kuwa shirika hilo linashirikiana na mamlak aya mawasiliano nchini TCRA katika  kubuni na kuweka mikakati ya utekelezaji wa mfumo wa anwani za makazi na postikodi

Katika hatua nyingine bwana Mndeme amesema hivi sasa shirika lake linataka kujiendesha kisasa zaidi ili kuzidi kuwashawishi vijana watumie huduma zao.

No comments:

Post a Comment