Kiungo mchezeshaji wa klabu ya Chelsea ya England amewaomba
radhi mashabiki wa soka kwa kitendo cha kumpiga teke kijana muokota mipira
katika mchezo kati ya timu yake na Swansea wa kusaka tiketi cha kucheza fainali
ya kombe la ligi la nchi hiyo Capital
One.
Hazard amesema kuwa nia yake haikuwa kumpiga teke
kijana huyo bali alichokuwa anataka ni kupiga mpira lakini kwa bahati mbaya
akampiga katika tumbo.
Kocha wa Chelsea Rafael benitez amesema kuwa suala
la hazard ambaye alioneshwa kadi nyekundu baada ya tukio hilo litajadiliwa
ndani ya klabu hivyo hawezi kulielezea kiundani.
Katika mchezo huo Chelsea ilikwenda suluhu na Swansea
hivyo kuondolewa katika michuano hiyo na kuifanya Swansea sasa kucheza na Bradford
katika mchezo wa fainali.
Anuary. BBC
No comments:
Post a Comment