Karibu katika blog yetu

Thursday, January 24, 2013

HAZARD AOMBA MSAHAMA KWA KUMPIGA TEKE MUOKOTA MIPIRA





 
Kiungo mchezeshaji wa klabu ya Chelsea ya England amewaomba radhi mashabiki wa soka kwa kitendo cha kumpiga teke kijana muokota mipira katika mchezo kati ya timu yake na Swansea wa kusaka tiketi cha kucheza fainali ya  kombe la ligi la nchi hiyo Capital One.

Hazard amesema kuwa nia yake haikuwa kumpiga teke kijana huyo bali alichokuwa anataka ni kupiga mpira lakini kwa bahati mbaya akampiga katika tumbo.

Kocha wa Chelsea Rafael benitez amesema kuwa suala la hazard ambaye alioneshwa kadi nyekundu baada ya tukio hilo litajadiliwa ndani ya klabu hivyo hawezi kulielezea kiundani.


Katika mchezo huo Chelsea ilikwenda suluhu na Swansea hivyo kuondolewa katika michuano hiyo na kuifanya Swansea sasa kucheza na Bradford katika mchezo wa fainali.

Anuary.                                    BBC

No comments:

Post a Comment