Karibu katika blog yetu

Wednesday, January 30, 2013

CAF WANAFURAHIA ZAMBIA KUTOLEWA- HERVE RENARD


Herve Renard




Baada ya kushuhudia timu yake ikiondolewa katika michuano ya kombe la mataifa ya Afrika mwaka huu, kocha mkuu wa Zambia Herve Renard amesema anajua fika kuwa shirikisho la soka Afrika Caf litakuwa na furaha baada ya waliokuwa mabingwa hao watetezi kuondolewa katika hatua ya makundi.

Renard amesema Caf walikuwa hawapendi kuona Zambia ikitetea ubingwa huo na hatimaye kushiriki kombe la mabara nchini Brazil kwa kuwa wanaamini kuwa Chipolopolo haichezi soka la kuvutia.

Kocha huyo raia wa Ufaransa ameongeza na kusema kuwa kutolewa kwao sio mwisho wa dunia hivyo wanatakiwa wajipange katika michuano ijayo.


Naye mlinda mlango wa Zambia Kennedy Mweene amewataka wachezaji wenzake wazidi kushikama katika kipindi hiki ili waweze kufanya vizuri katika michezo ya kuwania kufuzu kucheza kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment