Thursday, July 25, 2013
MPOTO ALIA NA BONGO FLAVOUR!
Mwanamuziki na mtunzi wa mashairi mahiri nchini Mrisho Mpoto amesema wasanii wengi wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Flavour) ni wafanyabiashara zaidi hivyo wanashindwa kutetea na kuitambulisha jamii ama hadhira inayowazunguka.
Mpoto amesema hayo na Mlimani TV wakati wa kongamano la Muziki wa Afrika lililoanza hii leo
(25/07/2013) idara ya sanaa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Msanii huyo anayejulikana kwa jina la "Mjomba" amesema kuwa tofauti na nchi kama Senegal ambayo ina Youssou n'dour na Marekani, Michael Jackson, Tanzania mpaka sasa hakuna msanii ambaye anaweza akawa kitambulisho cha sanaa ya muziki nchini.
Katika hatua nyingine, Mpoto amesema vyombo vya habari vinakabiliwa na changamoto kubwa ya kuutangaza muziki wa Tanzania ndani na nje ya nchi.
Kongamano la Muziki wa Afrika linaloendeshwa na idara ya sanaa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam linaendelea na linatarajia kufikia kilele chake siku ya jumamosi kwa wahadhiri, nguli mbalimbali wa muziki kutoka nchi mbalimbali duniani kuwasilisha mada kuhusiana na muziki.
Maxmillian John Ngube, Hawa, Shumu, Emmanuel Kihwelu
KAMERA YETU
Mkulima katika kijiji cha Chiwerere mkoani Lindi akipiga piga mahindi baada ya kuvuna |
Binti akiweka mahindi sehemu nzuri baada ya kuyavuna katika kijiji cha Chiwerere Lindi |
Daladala kutoka kijiji cha Kijiweni mpaka Lindi |
Mvuvi katika kijiji cha Kijiweni, Lindi |
Kijiji cha Tchezema kilichopo Mvomero mkoano Morogoro |
Sunday, July 14, 2013
TBS: HATUWEZI KUBAINI SIMU FEKI
Shirika la viwango nchini TBS limesema kuwa kwa sasa halina teknolojia inayowawezesha wataalamu wake kubaini simu zisizo na viwango ama feki.
Afisa uhusiano wa TBS, Bi Roida Andusanile akiongea na Mlimani TV amewataka wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho shirika lake linajipanga kuhakikisha inapata teknolojia hiyo ili kudhibiti uingizwaji wa simu hizo ambao umekuwa ukiongezeka kwa kasi katika maeoneo mengi nchini hususa katika jiji la Dar es Salaam.
Anuary Mkama.
Afisa uhusiano wa TBS, Bi Roida Andusanile akiongea na Mlimani TV amewataka wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho shirika lake linajipanga kuhakikisha inapata teknolojia hiyo ili kudhibiti uingizwaji wa simu hizo ambao umekuwa ukiongezeka kwa kasi katika maeoneo mengi nchini hususa katika jiji la Dar es Salaam.
Anuary Mkama.
Sunday, June 16, 2013
Sabri Lamouchi aikubali Stars!
Thomas Ulimwengu |
Nadir Haroub |
Sabri Lamouchi |
Juma Kaseja akijitahidi kuokoa mpira wa tuta uliopigwa na Yahya Toure |
Thomas Ulimwengu |
Juma Kaseja |
Kim Poulsen akimlalamikia kamisaa kuhusiana na penalty |
Kim Poulsen akiwalalamikia waaamuzi baada ya mapumziko |
kocha huyo kijana amesema kuwa amefurahishwa zaidi na uwezo wa washambuliaji wa Stars ambao walikuwa wanaliandama lango la timu yake kila mara.
Nao wachezaji wa Stars, Juma Kaseja, Frank Domayo, Mbwana Samatta, Nadir Haroub wameitaka serikali na TFF kuendelea kuipa maandalizi mazuri timu ya taifa kwa mashindano mengine yanayokuja.
Mbwana Samatta |
Akiongea zaidi Mbwana Samatta anayecheza katika klabu ya TP Mazembe ya DRC amesema kuwa nafasi anayocheza kwa sasa kama winga wa pembeni imekuwa ngumu kwake kutokana na kulazimika kurudi nyuma kusaidia safu ya ulinzi tofauti na anapokuwa katika klabu ya TP Mazembe, lakini amesema anafurahia kucheza kwani ni nafasi aliyokuwa anacheza awali lakini pia Kim Poulsen ndiyo nafasi anayopenda zaidi kumuona akicheza.
kutokana na matokeo hayo sasa, Ivory Coast imeungana na Ethiopia, Misri na Tunisia kutinga katika hatua ya mtoano ya kutafuta wawakilishi watano pekee ambao wataliwakilisha bara hili katika fainali za dunia za mwaka 2014 nchini Brazil.
Thursday, May 30, 2013
KUTOKA SAVE THE CHILDREN
Nchi
za Kusini mwa Jangwa la Sahara hatari kwa mtoto anayezaliwa- Taarifa ya Shirika
la Save the Children kuhusu Hali ya Wazazi Ulimwenguni - 2013
Save
the Children imezindua taarifa yake ya Hali ya Wazazi Ulimwenguni leo, 7 Mei,
2013 ikiwa na faharasa ya hatari ya kuzaliwa (Birthday Risk Index) ikionesha
kuwa nchi za Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara zinabaki kuwa ukanda hatari
kwa mtoto anayezaliwa.
Katika
taarifa hiyo,Tanzania iko katika nafasi ya 10 miongoni mwa nchi zenye idadi
kubwa ya vifo vinavyotokea siku ya kwanza ya kuzaliwa ulimwenguni. Kiafrika
Tanzania ni nchi ya tatu kwa vifo
vinavyotokea siku ya kwanza ya kuzaliwa baada ya Nigeria na DRC na kwa
ukanda wa Afrika mashariki inaongoza. Vilevile, Tanzania inachangia asilimia 2%
ya vifo vinavyotokea siku ya kwanza ya kuzaliwa ulimwenguni, ambavyo huchangiwa
zaidi na matatizo ya uzazi kabla ya muda wa kujifungua, ukosefu wa vifaa vya
kujifungulia, na changamoto za kupata huduma kwa watoto wachanga, hususani kwa
kina mama wanaoishi maeneo ya vijijini.
Tanzania imefanya mabadiliko makubwa ya kisera katika kupanua
huduma za afya kwa watoto wanaozaliwa. Pamoja na hilo, kwa mujibu wa taarifa
hii, watoto 17,000 hufa katika siku zao za kwanza za kuzaliwa na pia watoto
48,000 hufa kila mwaka, hivyo kuiweka Tanzania miongoni mwa nchi 10
zinazoongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya vifo vya watoto wach
anga,” anasema Dk.
Stephen Ayella, Mshauri wa Programu ya Afya wa Save the Children nchini
Tanzania.
Somalia,
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC), Mali, Sierra Leone, zina idadi kubwa
zaidi ya vifo vya watoto wachanga ulimwenguni. Mathalani, kwa mujibu wa taarifa
hiyo, nchini Somalia, mtoto anayezaliwa yuko katika hatari ya kufa mara 40
zaidi kuliko mtoto aliyezaliwa Luxembourg. Vifo vya watoto wachanga, hususani
katika siku ya kwanza ya kuzaliwa ni ishara hali ya usalama wa wazazi kutokana
na matatizo ya wakati wa kujifungua na hali ya mtoto mchanga ndani ya masaa 24
baada ya kuzaliwa.
Ulimwenguni
kote, watoto milioni moja hufa kila mwaka katika siku yao ya kwanza ya kuzaliwa
ama kwa lugha nyingine watoto wawili hufa kila dakika, hivyo kuifanya siku ya
kwanza kuwa siku ya hatari zaidi kwa maisha ya mtu karibu katika kila nchi
ulimwenguni.
Takwimu
za kitaifa zilizotolewa katika faharasa zinaangazia nchi nyingi ulimwenguni.
Viashiria kama hatari za vifo wakati wa uzazi, vifo vya watoto chini ya miaka
5, idadi itarajiwayo ya miaka ya mahudhurio katika shule rasmi, pato la taifa
na ushiriki wa wanawake katika uongozi wa serikali vimetumika katika kupanga
nafasi. Kati ya nchi 176 ulimwenguni, Tanzania ni nchi ya 135, ikionesha
kupanda kidogo ukilinganisha na mwaka jana ambapo ilishika nafasi ya 140.
Taarifa
imebainisha mambo ya msingi yanayochangia katika idadi hiyo kubwa barani
Afrika. Mambo hayo ni pamoja na idadi kubwa ya watoto wanaozaliwa kabla ya
kutimiza muda, kama ilivyo katika mfano wa Malawi ambayo ina idadi kubwa ya
watoto wanaozaliwa kabla ya kutimiza muda na ambao wanazaliwa na uzito pungufu.
Mambo mengine ni pamoja na afya duni za wazazi, uzazi katika umri mdogo,
ambavyo vinawaweka wazazi katika hatari ya kupata matatizo wakati ya uzazi
yakiwa ni pamoja na mtoto aliye tumboni kutokuwa katika kiwango kinachostahili
na kuzaa kabla ya muda.
Mkurugenzi wa
Save the Children wa Ukanda wa Afrika Magharibi na Kati, Natasha Quist, anasema:
“Nchi za Afrika na jumuiya ya ulimwengu wanafanya juhudi za kumaliza vifo vya
watoto vinavyoweza kuzuilika, hata hivyo kama tunataka kufikia lengo hili la
kihistoria, kunahitajika juhudi za ziada kuelekezwa katika kunusuru maisha ya
watoto katika siku na miezi yao ya kwanza ya kuzaliwa.”
Wataalam wa
masuala ya watoto wachanga wanakiri kuwa maendeleo makubwa yangeweza kufanyika
kwa kueneza mbinu rahisi, zenye tija na gharama ndogo na kubadilishana mifano
bora katika bara hilo.
Kupitia miradi
yake ya Kuokoa Maisha ya Watoto Wachanga (SNL) na MAISHA, Save the Children nchini Tanzania imekuwa mstari wa mbele nchini
katika kuanzisha na kufuatilia huduma za Malezi kwa Mtindo wa Kangaroo (KMC),
mtindo ambao ni maalum kwa kutunza watoto njiti na wenye uzito pungufu. Kwa
kushirikiana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Save the Children imeanzisha
vituo 27 vya Malezi ya Mtindo wa Kangaroo Tanzania bara na Visiwani. Pia
imefundisha zaidi ya wauguzi na madaktari 973 pamoja na kuwaelekeza juu ya
Mtindo wa Kangaroo wafanyakazi 1185 wa kada zingine za afya.
Save the
Children inakadiria kuwa maisha ya watoto wachanga milioni moja yanaweza
kuokolewa kila mwaka, kuhakikisha upatikanaji wa vitu vinne tu ambavyo gharama
yake ni ndogo: sindano za Corticosteroid kwa kina
mama walio katika uchungu wa kabla ya muda, ambazo ni muhimu katika kupunguza
vifo vitokanavyo na matatizo ya kupumua kwa watoto wanaozaliwa; vifaa vya
kuamsha watoto wanaoshindwa kupumua baada ya kuzaliwa; dawa ya kusafishia baada
ya kondo kutoka ili kuzuia maambukizi yanayotokana na kondo la nyuma na madawa
ya sindano za kuzuia matatizo ya kuvimba
na kifua kwa watoto.
Vilevile,
katika taarifa hiyo, Save the Children inaendelea kuonesha uhusiano kati ya
afya ya mama mjamzito na vifo vya watoto wachanga. Faharasa hiyo ya Hali ya
Wazazi Ulimwenguni inapanga huduma ambazo kila nchi inazitoa kwa kina mama
kulingana na viashiria vya afya ya mama mjamzito, watoto chini ya miaka mitano,
kiwango cha elimu kwa kina mama, kipato na hali ya kisiasa. Finland inaongoza
ambapo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo inashika mkia.
Save
the Children inatoa wito ufuatao kwa viongozi ulimwenguni:
§ Kuwekeza katika mambo yenye gharama
nafuu na ambayo yanaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo vya watoto wachanga. Madawa
yanayoweza kutibu ama kuzuia maambukizi madogo madogo ambayo yanaweza
kusababisha vifo. Vilevile kuhimiza unyonyeshaji wa maziwa ya mama pekee na malezi
ya Mtindo wa Kangaroo, mambo ambayo hayana gharama yoyote, lakini yanaweza
kuokoa maisha ya maelfu ya watoto.Vilevile, wahudumu wa kina mama wanaojifungua
wanapaswa kupewa mafunzo, msaada na vifaa vya kutosha ili waweze kutoa huduma
kwa ufasaha.
§ Kuimarisha mifumo ya afya ili kina mama wengi zaidi waweze
kufikiwa na wahudumu wa afya wenye ujuzi. Kuwekeza zaidi katika wahudumu wanaopokea wagonjwa
na wahudumu wa afya katika jamii ili kuweza kusaidia kuwafikia kina mama na
watoto walio katika hatari zaidi.
.
§ Kupambana na viini vya
vifo vya watoto wachanga, usawa wa kijinsia na utapiamlo. Kusaidia kina mama kuwa na nguvu na imara-kimwili, kifedha na
kijamii kunasaidia kuwawezesha watoto wao pia kuwa na nguvu na kuweza kuishi na
kukua.
Dk.
Rachel Makunde, Meneja Programu ya Afya ya Mama Wajawazito na Watoto wa Save
the Children nchini Tanzania anatoa wito kwa serikali kuelekeza nguvu zaidi
katika mipango na bajeti kwa ajili ya kuokoa maisha ya watoto, ikiwa ni pamoja
na kueneza huduma ya Malezi kwa Mtindo wa Kangaroo hadi hospitali za wilaya na
katika vituo vya afya.
“Kuzaliwa kabla ya muda kunachangia vifo vya watoto wachanga kwa
asilimia 35, kwa hivyo afua zenye kulenga watoto njiti zinaweza kuchangia kwa
kiasi kikubwa kupunguza vifo vya watoto,” anasema.
Tuesday, May 28, 2013
Kongo yagawika pendekezo la Rais Kikwete
Pendekezo
la Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania kwa serikali ya Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo izungumze na makundi ya waasi na nchi jirani
kutatua mzozo wa mashariki ya nchi hiyo linaonekana kuwagawa Wakongo.
Kwenye
mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kinshasa, kuna mwangwi wa
sauti za Wakongomani wakiupongeza msimamo wa Rais Kikwete kwamba kuweko
na mtazamo wa ujumla katika kutafuta ufumbuzi wa mzozo wa kanda ya
Maziwa Makuu.
Mwandishi
wetu wa Kinshasa anaripoti kwamba wakaazi wengi wa mji huo wanaamini
kuwa pendekezo hilo la Rais Kikwete linaweza kusaidia amani ya kudumu.
Kwenye
mkutano wa marais 11 wa Nchi za Maziwa Makuu kwa ajili ya Kongo
uliotishwa kando ya mkutano wa Umoja wa Afrika, mjini AddisAbaba, Rais
Kikwete alipendekeza kufanyike mazungumzo baina ya Kongo na kundi la
waasi la M23, Rwanda na kundi la waasi la FDLR na Uganda na waasi wake
wa ADF/Nalu kwa ajili ya amani ya kudumu ya kanda ya Maziwa Makuu.
Tanzania inachangia wanajeshi 1,280 kwenye kikosi maalum cha Umoja wa Mataifa mashariki mwa Kongo,
Umoja usio wa kawaida Kinshasa
Pendekezo
hili limezua kile mwandishi wetu wa Kinshasa anachokiita “tukio la
nadra kabisa nchini Kongo“ kwa wabunge wa upinzani na wale wa chama
tawala kuwa na kauli moja kuhusu maswala muhimu ya kitaifa.
Rais
Kikwete amefanikiwa kuwaelekeza wanasiasa wa Kongo kuchukuwa msimamo wa
pamoja kuhusu juhudi za kutafuta suluhisho la kudumu kwenye kanda ya
Maziwa Makuu.
Kwa
mujibu wa taarifa za mashirika ya habari ni kwamba Rais Kikwete
aliwambia maraisi wenzake pamoja na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban
Ki-moon, na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika Afrika, kwamba
ni lazima kuweko na mtizamo wa ujumla kwa ajili ya kumalizisha machafuko
ya miaka mingi kwenye kanda la Maziwa Makuu.
Kwa
hiyo Rais Kikwete alipendekeza Kongo kuendesha mazungumzo na waasi wa
M23, na vilevile kuitaka Rwanda kuzungumza na waasi wa FDLR na Uganda
kufungua mazungumzo na waasi wake wa ADF/Nalu. Pendekezo hilo
limepongezwa na upinzani na chama tawala nchini Kongo, akiwemo mbunge
Justin Bitakwira, ambaye ni kiongozi wa wabunge wa upinzani wa UNC.
Naye
Franklin Tshamala, msemaji wa muungano wa vyama tawala, amesema kwamba
pendekezo hilo la Rais Kikwete ni hatua ya ujasiri ya kutaka kurekebisha
mitizamo tofauti waliyonayo viongozi wa mataifa haya matatu.
Rwanda yakataa
Pendekezo
hilo la Rais wa Tanzania lilipongezwa pia na serikali ya Kongo. Akiwa
mjini Addis Ababa, Waziri wa Mambo ya Nje ya Kongo, Raymond Tshibanda,
aliiambia Radio France Internationale kwamba msimamo huo unalingana na
ombi la miaka mingi la serikali ya Kongo kwa majirani zake.
Lakini
Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Louise Mushikiwabo, aliyehojiwa na
redio hiyo hiyo alisema matamshi hayo ya Rais Kikwete ni ya upotofu na
nchi yake haiwezi kamwe kuzungumza na watu waliohusika na mauwaji ya
halaiki.
Magazeti
mengi ya siku ya Jumanne (tarehe 28 Mei) yamezungumzia matamshi ya Rais
Kikwete na maoni ya wananchi wa Kongo. Gazeti Lavenir limechapisha
kichwa cha habari kwa wino mzito kikimuita Rais Kikwete ”Jjasiri wa
kanda ya Maziwa Makuu.”
Kwenye
ukarasa wa mwanzo, gazeti la upinzani la Tempetes des Tropiques
limeandika “Kikwete arusha bomu Addis Abeba”, likiyaelezea matamshi ya
Rais Kikwete kuwa sawa na bomu alilowarushia marais wenzake ambao kwa
muda mrefu wameonyesha unafiki katika kumaliza machafuko ya Maziwa Makuu
kwa zaidi ya miaka 20 sasa.
Goma hawataki mazungumzo na M23
Lakini
hali ikiwa hivyo mjini Kinshasa, kwenye eneo la mashariki ya Kongo,
ambako ndiko hasa kwenye mgogoro kati ya serikali na waasi wa M23, maoni
ni tafauti.
Mwandishi
wetu wa Goma, John Kanyunyu, anaripoti kwamba mashirika ya kiraia ya
huko yamekataa mazungumzo baina ya serikali ya DRC na wajumbe wa M23.
Makamu mwenyekiti wa mashirika ya hayo kiraia katika mkoa wa Kivu ya Kaskazini, ambaye pia ni msemaji wa mashirika hayo, Omar Kavota, amesema “hakuna tena la kuzungumza, kwani tayari mkataba wa M23 baina ya chama cha zamani cha uasi CNDP umeshajadiliwa.”
Kauli hiyo ya mashirika ya kiraia inakuja baada ya pendekezo la Rais Kikwete mbele ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na marais wa kanda ya Maziwa Makuu kuiomba serikali kurudi kwenye meza ya mazungumzo baina yake na waasi wa M23.
Aidha
kauli hiyo ya mashirika ya kiraia ya kuitaka serikali kutozungumza na
wajumbe wa M23, inachochewa pia na utendaji kazi wa wanajeshi wa
serikali katika uwanja wa mapigano.
Katika vita baina ya jeshi la serikali, FARDC, na waasi wa M23, jeshi hilo la serikali linatajwa kuwa, lilifaulu kwa mara ya kwanza kabisa, kuwazuia waasi wa M23 kuuteka upya mji wa Goma.
Kavota anasema ni bora zaidi kuwapatia nafasi ya kufanya kazi zao wanajeshi wa kikosi maalumu cha Umoja wa Mataifa kinachowajumuisha wanajeshi kutoka Tanzania, Malawi na Afrika ya Kusini.
Katika
kuwapongeza wanajeshi wa serikali kwa kazi waliyoifanya wakati wa
mapigano ya wiki iliyopita, mashirika ya wanawake kutoka asasi za kiraia
na vyama vya kisiasa, wametoa mchango wa pesa wa kile walichokiita
“kuwanunulia wanajeshi wa serikali maji ya kunywa.”
Ripoti hii imetayarishwa na Saleh Mwanamilongo, Kinshasa, na John Kanyunyu, Goma
Mhariri: Mohammed Khelef
Mhariri: Mohammed Khelef
Friday, April 19, 2013
KUTOKA TFF
MECHI YA MGAMBO, YANGA YAINGIZA MIL 24/-
Mechi
ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Mgambo Shooting na Yanga iliyochezwa
jana (Aprili 17 mwaka huu) Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga imeingiza
sh. 24,865,000 kutokana na watazamaji 4,386.
Viingilio
katika mechi hiyo namba 162 iliyomalizika kwa timu hizo kutoka sare ya
bao 1-1 vilikuwa sh. 10,000 kwa jukwaa kuu na sh. 5,000 huku kila klabu
ikipata mgawo wa sh. 5,547,337.50 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani
(VAT) iliyolipwa ni sh. 3,792,966.10.
Asilimia
15 ya uwanja sh. 2,820,680.08, msimamizi wa kituo sh. 120,000, kamishna
wa mechi sh. 90,000, waamuzi sh. 270,000, maandalizi ya uwanja sh.
100,000 na tiketi sh. 1,587,500.
Mgawo
mwingine ni gharama za mechi sh. 1,692,408.05, Kamati ya Ligi sh.
1,692,408.05, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 846,204.05
na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga (TRFA) sh. 658,158.69.
MAKOCHA AZAM, FAR RABAT KUTETA
Makocha
wa timu za Azam, Stewart John Hall na AS FAR Rabat ya Morocco,
Abderazzak Khairi watakutana na waandishi wa habari kesho (Aprili 19
mwaka huu) kuzungumzia mechi yao itakayofanyika Jumamosi, Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam.
Mkutano
huo ambao pia utawahusisha manahodha wa timu hizo mbili utafanyika saa 5
kamili asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania
(TFF) zilizoko Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Barabara ya Uhuru na
Shaurimoyo.
Timu
hizo zitakutana katika mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili ya Kombe
la Shirikisho itakayoanza saa 10 kamili jioni. Mechi ya marudiano
itachezwa nchini Morocco wiki mbili baadaye.
JKT RUVU, YANGA KUUMANA JUMAPILI
Yanga
ambayo inafukuzia kwa karibu taji la Ligi Kuu ya Vodacom itapambana na
JKT Ruvu katika mechi pekee ya ligi hiyo wikiendi hii itakayofanyika
Jumapili (Aprili 21 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mbali
ya mechi hiyo, nyingine zitakazochezwa mwezi huu ni kati ya African
Lyon na JKT Ruvu itakayofanyika Aprili 24 kwenye Uwanja wa Chamazi, Dar
es Salaam wakati Aprili 25 ni kati ya Ruvu Shooting na Simba kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Nayo
Coastal Union itaikaribisha Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini
Tanga katika mechi itakayochezwa Aprili 27. Uwanja wa Taifa utakuwa
mwenyeji wa mechi kati ya Simba na Polisi Morogoro itakayofanyika Aprili
28.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Thursday, April 11, 2013
WALIMU WAPINGA MPANGO WA SERIKALI KUSHUSHA ALAMA ZA UFAULU
Kufuatia kauli ya Naibu Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Philipo Mulugo kusema kuwa serikali inakusudia kushusha alama za ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha nne kuelekea kidato cha tano na cha sita, wananchi pamoja na baadhi ya walimu ambao hawakupenda kutajwa majina yao wamesema kuwa njia hiyo sio suluhisho la kuinua elimu nchini bali kuzidi kudidimiza.
Wakiongea mjini hapa Kigoma, wamesema kushusha huko alama kutakuwa kunamfurahisha mwanafunzi na wazazi wake katika makaratasi huku mwanafunzi huyo kichwani hakiwa hajaelimika vya kutosha.
Wameongeza na kusema serikali inatakiwa kuhakikisha inatafutia ufumbuzi wa kudumu matatizo ya elimu yaliyopo kama nyezo za kufundishia, kuongeza idadi ya walimu sanjari na mishahara pamoja na ujenzi wa nyumba zao.
Akiongea katika mkutano na wamiliki wa shule za sekondari nchini uliofanyika mjini Mbeya, Naibu waziri Mulugo amesema kuwa mpango huo wa kushusha alama ya ufaulu kwa kidato cha nne utasaidia kutoa nafasi zaidi kwa wanafunzi kupata nafasi ya kusoma kidato cha tano na cha sita.
Wakiongea mjini hapa Kigoma, wamesema kushusha huko alama kutakuwa kunamfurahisha mwanafunzi na wazazi wake katika makaratasi huku mwanafunzi huyo kichwani hakiwa hajaelimika vya kutosha.
Wameongeza na kusema serikali inatakiwa kuhakikisha inatafutia ufumbuzi wa kudumu matatizo ya elimu yaliyopo kama nyezo za kufundishia, kuongeza idadi ya walimu sanjari na mishahara pamoja na ujenzi wa nyumba zao.
Akiongea katika mkutano na wamiliki wa shule za sekondari nchini uliofanyika mjini Mbeya, Naibu waziri Mulugo amesema kuwa mpango huo wa kushusha alama ya ufaulu kwa kidato cha nne utasaidia kutoa nafasi zaidi kwa wanafunzi kupata nafasi ya kusoma kidato cha tano na cha sita.
KOCHA RHINO APIGWA FAINI, AFUNGIWA MECHI SITA
KAMATI
ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imempiga faini
ya sh. 400,000 na kumfungia mechi sita Kocha wa Rhino Rangers, Renatus
Shija kwa kushiriki vitendo vinavyoashiria imani za ushirikina na
kumdhihaki mwamuzi kwenye mechi za Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Adhabu
hizo zimetolewa kwa mujibu wa kifungu cha 31(1)(a) na (b) cha Kanuni za
FDL ambapo Kocha huyo aliyeipandisha daraja Rhino Rangers kucheza Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) alifanya vitendo hivyo kwenye mechi mbili tofauti.
Mechi
hizo ni kati ya Kanembwa JKT na Rhino Rangers iliyochezwa Februari 23
mwaka huu Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma, na ile kati ya Rhino
Rangers na Morani iliyochezwa Machi 17 mwaka huu Uwanja wa Ali Hassan
Mwinyi mjini Tabora.
Pia
klabu ya Rhino Rangers imepigwa faini ya sh. 200,000 kutokana na Polisi
Wanajeshi- MP kuwapiga walinzi milangoni kwenye mechi hiyo dhidi ya
Kanembwa JKT ili kupisha washabiki wa timu hiyo waingie bure uwanjani.
Mchezaji
wa timu ya Pamba ya Mwanza, Leonard Nahole amepigwa faini ya sh.
200,000 na kufungiwa mechi nne baada ya kumrushia chupa ya maji mwamuzi
kwa madai amependelea kwenye mechi dhidi ya Polisi Tabora iliyochezwa
Machi 16 mwaka huu.
Nao
wachezaji Joseph Mapalala, Yohana Mirobo, Noel Makunja, Mkome Pastory
na Rudenzi Kilinga wa Polisi Mara wamepigwa faini ya sh. 200,000 kila
mmoja na kufungiwa mechi tatu kwa kufanya vitendo vinavyoshiria
ushirikina na kumkimbiza mwamuzi kwenye mechi dhidi ya Morani
iliyochezwa Machi 9 mwaka huu. Adhabu za wachezaji hao ni kwa mujibu wa
kifungu cha 27(1)(g) cha Kanuni za FDL.
Klabu
ya Villa Squad imepigwa faini ya sh. 150,000 kwa kuchelewa uwanjani
kwenye mechi yake dhidi ya Ashanti United wakati Majimaji imepigwa faini
ya sh. 200,000 kutokana na washabiki wake kufanya vurugu kwenye mechi
dhidi ya Mbeya City iliyochezwa Uwanja wa Majimaji.
Vilevile
Msimamizi wa Uwanja wa Majimaji aliyetambulika kwa jina moja la Mapunda
aliwatukana waamuzi kwenye mechi hiyo, na suala lake litafikishwa
kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa ajili ya hatua za kinidhamu.
Pia
uongozi wa Uwanja wa Mafinga unaotumiwa na timu ya daraja la kwanza ya
Kurugenzi umetakiwa kuufanyia marekebisho, vinginevyo hautatumika kwa
mechi za FDL msimu ujao.
Tuesday, April 9, 2013
Kigoma yakabiliwa na uhaba wa walimu wa sayansi.
Imeelezwa kuwa mkoa wa Kigoma unakabiliwa na upungufu mkubwa wa walimu wa somo la sayansi hali ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi wa kidato cha nne na sita kushindwa kufanya vizuri katika mitihani yao ya taifa.
kauli hiyo imetolewa na Afisa elimu msaidizi wa Kigoma bwana Venance Babukege wakati akizungumzia maendeleo ya elimu ya mkoa huo.
Bwana Babukege amesema idadi wa walimu wa masomo ya sanaa inaridhisha huku upande wa sayansi hali ni mbaya zaidi hivyo kusababisha wanafunzi wengi wasichague michepuo ya masomo hayo huku wale waliochagua nao wakipata matokeo ambayo hayaridhishi.
kwa upande wa walimu wanaofundisha masomo ya sayansi, babukege amesema wamekuwa wakiomba uhamisho pindi wanapopangiwa kigoma kutokana na kukosekanika nyenzo za kufundishia kwa vitendo.
katika mipango ya kujipanga kuhakikisha kiwango cha ufaulu kinaongezeka hususa kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka huu, Babukege amesema kuwa hivi sasa kitengo chake kinatembelea katika shule zote za sekondari za mkoa kuzungumza na walimu ili kupata njia ambazo zitasaidia kuinua kiwango cha ufaulu.
Anuary- Kigoma.
kauli hiyo imetolewa na Afisa elimu msaidizi wa Kigoma bwana Venance Babukege wakati akizungumzia maendeleo ya elimu ya mkoa huo.
Bwana Babukege amesema idadi wa walimu wa masomo ya sanaa inaridhisha huku upande wa sayansi hali ni mbaya zaidi hivyo kusababisha wanafunzi wengi wasichague michepuo ya masomo hayo huku wale waliochagua nao wakipata matokeo ambayo hayaridhishi.
kwa upande wa walimu wanaofundisha masomo ya sayansi, babukege amesema wamekuwa wakiomba uhamisho pindi wanapopangiwa kigoma kutokana na kukosekanika nyenzo za kufundishia kwa vitendo.
katika mipango ya kujipanga kuhakikisha kiwango cha ufaulu kinaongezeka hususa kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka huu, Babukege amesema kuwa hivi sasa kitengo chake kinatembelea katika shule zote za sekondari za mkoa kuzungumza na walimu ili kupata njia ambazo zitasaidia kuinua kiwango cha ufaulu.
Anuary- Kigoma.
Monday, April 8, 2013
TABORA NA MASOMO YA JIONI KWA KIDATO CHA NNE
Mkoa wa Tabora umeamua kutoa nafasi za masomo ya jioni kwa wanafunzi waliofeli kidato cha nne hivi karibuni ili kuwapa nafasi waweze kusawazisha makosa yao na hatimaye waendelee na masomo ya ngazi ya juu.
Afisa elimu wa mkoa huo Midamo Paul Makungu amesema kuwa ofisi yake imeshakubaliana na walimu wa shule za sekondari kuanzisha masomo hayo kwa wanafunzi watakaopenda.
Afisa elimu wa mkoa huo Midamo Paul Makungu amesema kuwa ofisi yake imeshakubaliana na walimu wa shule za sekondari kuanzisha masomo hayo kwa wanafunzi watakaopenda.
Monday, March 25, 2013
Dk. Ali Mohamed Shein akutana na Mhe. Xi
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk. Ali Mohamed Shein amefanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China
Mhe. Xi Jinping na kumueleza kuwa Zanzibar imefungua milango ya uwekezaji hivyo
China inaweza kutumia fursa hiyo kwa kuekeza katika sekta mbali mbali za
kimaendeleo.
Dk. Shein aliyasema hay leo wakati alipokuwa na mazungumzo
na Rais wa China Mhe. Xi Jinping huko katika ukumbi wa hoteli ya Serena Jijini
Dar-es-Salaam.
Katika maelezo yake Dk. Shein alimueleza Rais Xi Jinping kuwa Tanzania ikiwemo Zanzibar
inathamini uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya pande mbili hizo na
kusisitiza kuwa ziara yake hiyo itakuwa ni fursa ya pekee ya kuweza kuitangaza
Zanzibar katika sekta ya uwekezaji ili Zanzibar nayo inufaike.
Alisema kuwa Zanzibar imeweka mazingira mazuri ya uwekezaji
hivyo inaikaribisha China kuja kuekeza Zanzibar
kwa lengo la kuzidi kuimarisha uhusiano
wa kidugu na wa kihistoria uliopo kati ya pande mbili hizo.
Dk. Shein alitoa shukurani na pongezi kwa China kutokana na
kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika sekta mbali mbali za kimaendeleo kwa
kutambua mchango wake mkubwa hasa ikizingatiwa kuwa China ni miongoni mwa nchi
za mwanzo zilizotambua Mapinduzi ya
Zanzibar ya mwaka 1964.
Alisema kuwa China imeweza kuunga mkono sekta mbali mbali za
maendeleo na kusifu kazi nzuri inayofanywa na madaktari wa nchi hiyo ambao
wanafanya kazi zao katika hospitali za Zanzibar pamoja na kusifu mchango wa
nchi hiyo katika ujenzi wa hospitali ya Abdala Mzee kisiwani Pemba.
Dk. Shein alieleza kuwa China imeweza kusaida miradi mbali
mbali ikiwa ni pamoja na kuipatia Zanzibar mikopo nafuu katika kuendeleza
miradi ukiwemo mradi wa maji safi na
salama mnamo miaka ya 70, misaada katika sekta ya habari, nafasi za masomo,
afya, miundombinu, ujenzi wa jengo la abiria la uwanja wa ndege wa Kimataifa wa
Abeid Karume unaoendelea, mawasiliano na miradi mengineyo.
Stars yamuweka matatani Taoussi
Majaliwa ya kocha mkuu wa Morocco Rachid Taoussi kuendelea kuifundisha timu ya taifa ya nchi hiyo yapo mashakani baada ya wadau wa soka wa Morocco kutaka kocha huyo ajiuzuru kutokana na kufungwa goli 3-1 na Tanzania katika mchezo wa kuwania kucheza kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil.
Wadau hao wa soka nchini humo wamesema kuwa kocha huyo ameshindwa kuiletea timu yao mafanikio lakini wameponda pia kitendo chake cha kufanya mabadiliko makubwa katika kikosi kilichocheza katika michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika na kile kilichopata kipigo cha aibu kutoka kwa Tanzania.
Morocco sasa inahitaji miujiza ili isonge mbele katika hatua nyingine ya kuwania nafasi ya kucheza fainali zijazo za dunia nchini Brazil.
Wadau hao wa soka nchini humo wamesema kuwa kocha huyo ameshindwa kuiletea timu yao mafanikio lakini wameponda pia kitendo chake cha kufanya mabadiliko makubwa katika kikosi kilichocheza katika michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika na kile kilichopata kipigo cha aibu kutoka kwa Tanzania.
Morocco sasa inahitaji miujiza ili isonge mbele katika hatua nyingine ya kuwania nafasi ya kucheza fainali zijazo za dunia nchini Brazil.
Saturday, February 2, 2013
HOTUBA YA RAIS
HOTUBA
YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA,
MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, KWA WANANCHI, TAREHE 31 JANUARY, 2013
Utangulizi
Ndugu Wananchi;
Kama ilivyo ada naomba
tuanze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, Mwenye Rehema, kwa kutujaalia uzima na
kutuwezesha kuzungumza kwa mara
nyingine kwa kutumia utaratibu wetu huu mzuri wa mawasiliano baina ya Rais na
wananchi wa Tanzania kila mwisho wa mwezi.
Siku ya leo nitazungumzia safari yangu ya Ufaransa, Uswizi na
Ethiopia. Pia nitazungumzia ujenzi wa bomba
la kusafirisha gesi asili kutoka Mtwara kuja Dar es Salaam.
Safari za Kikazi Nje ya Nchi
Ndugu Wananchi;
Safari
yangu ya Ufaransa, Uswizi na Ethiopia ilikuwa na manufaa makubwa kwa nchi
yetu. Nchini Ufaransa licha ya
kuimarisha uhusiano wa kirafiki baina ya nchi zetu, tumepata wawekezaji wengi
wakubwa wenye nia thabiti ya kuja kuwekeza hapa nchini. Pia tumekubaliana kuanza mazungumzo ya kuwa
na mpango mwingine wa ushirikiano.
Mpango wetu wa sasa ulioanza mwaka 2006 uliisha mwaka 2010. Mpango ule ulitusaidia sana kuboresha huduma
za maji katika miji ya Utete mkoani Pwani na Mpwapwa mkoani Dodoma.
Katika
mkutano wa Kongamano la Uchumi wa Dunia uliofanyika Davos, Uswizi,
tumehakikishiwa ushirikiano katika kuendeleza juhudi zetu za kuleta mapinduzi
ya kijani ili tujihakikishie usalama wa chakula na kupunguza umaskini vijijini
na kukuza uchumi wa nchi yetu. Aidha,
tulipata bahati ya kushirikishwa katika mjadala wa kuanzishwa kwa programu
kubwa ya kuzisaidia nchi za Afrika kutatua matatizo ya upatikanaji wa umeme. Naamini programu hiyo ikitekelezwa na wakubwa
kuheshimu kauli na ahadi zao itakuwa msaada mkubwa kwa maendeleo ya nchi za
Afrika zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Ndugu Wananchi;
Nchini
Ethiopia tulishiriki katika mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa
Afrika na katika kikao cha African Peer Review Mechanism (APRM) ambapo taarifa ya
tathmini ya utawala bora ya Tanzania na Zambia iliyofanywa na APRM ilijadiliwa. Kwa jumla hatuna mahali tuliponyooshewa
kidole kuwa tunafanya vibaya. Tumepongezwa
katika mambo mengi na tumepewa ushauri kwa baadhi ya maeneo waliyoona hatuna
budi kuyaboresha. Nilipata nafasi ya kusema
ambayo niliitumia kufafanua baadhi ya mambo yaliyokuwamo kwenye taarifa. Niliwashukuru na kuahidi kuufanyia kazi
ushauri uliotolewa. Tathmini ya nchi
yetu ilipitishwa kwa kauli moja.
Vurugu
za Kupinga Gesi Kusafirishwa Kutoka Mtwara
Ndugu wananchi;
Kama
mtakavyokumbuka tarehe 8 Novemba, 2012 kule Kinyerezi, Wilaya ya Ilala hapa Dar
es Salaam, niliweka jiwe la msingi la ujenzi wa bomba la kusafirisha gesi asili
kutoka Mtwara na Songosongo kuja Dar es Salaam.
Karibu na mwishoni mwa Desemba, 2012 kukafanyika maandamano mjini Mtwara
kupinga ujenzi wa bomba hilo. Katika
maandamano yale na baadaye kwenye kauli za wanasiasa na wanaharakati yakatolewa
madai kuwa gesi hiyo itumike kwa maendeleo ya Mtwara na kwamba yale
yanayotakiwa kufanyika Dar es Salaam yafanyike Mtwara. Pia, zilitolewa shutuma nyingine dhidi ya
Serikali eti kuwa kwa miaka mingi imewasahau na haiwajali wananchi wa Mikoa ya
Kusini na ujenzi wa bomba hilo ni muendelezo wa hayo. Kauli mbalimbali za
wanasiasa na wanaharakati ni kama vile ziliongeza mafuta kwenye kaa la moto na
kuuchochea mpaka kukatokea matukio yaliyotusikitisha na kutshtua sote. Baadhi ya ndugu zetu wamepoteza maisha na
mali za watu na Serikali kuharibiwa.
Ndugu Wananchi;
Katika hotuba
yangu ya kuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013, tarehe 31 Desemba, 2012,
nililisemea jambo hili. Leo mwezi mmoja
baadae, napenda kusisitiza mambo mawili.
Kwanza kwamba, si kweli kuwa Serikali inapuuza Mikoa ya Kusini. Na pili, kwamba kujenga bomba la kuipeleka gesi
Dar es Salaam hakuinyimi Mikoa ya Mtwara na Lindi fursa ya kunufaika na gesi iliyopo
Mtwara.
Ndugu Wananchi;
Serikali imefanya, inafanya
na ina mipango ya kufanya mambo mengi mazuri kwa ajili ya kuleta maendeleo katika
Mikoa ya Mtwara na Lindi. Ipo mipango ya
kuboresha miundombinu, huduma za kiuchumi na kijamii pamoja na kukuza uchumi
ikiwa ni pamoja na ujenzi wa viwanda vikubwa na vidogo. Serikali ya Awamu ya Tatu chini ya uongozi wa
Rais Mstaafu, Mheshimiwa Benjamin Mkapa, ilijenga daraja katika Mto Rufiji
maarufu kama Daraja la Mkapa. Hii
ilikuwa ni hatua kubwa ya awali katika safari ya kutatua matatizo ya usafiri ya
Mikoa ya Kusini. Serikali ninayoiongoza
mie iliachiwa kazi ya kukamilisha ujenzi wa barabara za lami kufikia darajani
na kuunanisha Mkoa wa Mtwara na Mkoa wa Ruvuma.
Kazi hiyo, tumeitekeleza vizuri na sasa tunakaribia kuimaliza. Tulikamilisha ujenzi wa barabara ya kutoka
Mnazi-Mmoja hadi Nangurukuru. Mwaka 2009
tukaanza ujenzi wa barabara ya kilomita
56 kutoka Somanga hadi Ndundu (darajani).
Ujenzi wa kilometa 36 za
mwanzo ulienda vizuri. Bahati mbaya
ujenzi wa kilomieta 20 za mwisho
umechelewa sana kwa sababu ya mmiliki wa kampuni iliyokabidhiwa kufanya kazi
hiyo kufariki. Kwa sababu hiyo, kampuni
ilipata mtikisiko kiasi na kusababisha kazi kutotekelezwa kwa kasi
tuliyoitarajia. Sasa mambo yametengemaa
na kazi inaendelea kwa kasi nzuri.
Matumaini yetu ni kuwa ifikapo mwezi Desemba, 2013 kazi hiyo itakuwa
imekamilika.
Hali
kadhalika, Rais Mstaafu, Mzee Benjamin Mkapa alituachia jukumu la kumaliza
ujenzi wa Daraja la Umoja katika mto Ruvuma na ujenzi wa barabara ya lami
kuanzia Mikoa ya Mtwara na Ruvuma.
Tumelikamilisha Daraja hilo na ujenzi wa barabara ya lami kutoka Masasi hadi
Mangaka umekamilika. Mchakato wa kujenga
barabara ya kwenda Songea na kwenda Darajani umefikia mahala pazuri. Tenda ya ujenzi wa barabara kutoka Tunduru
hadi Mangaka mpaka Darajani imeshatangazwa.
Kama mambo yataenda sawa miezi mitatu ijayo mjenzi atapatikana. Wakati huo huo ujenzi wa barabara kutoka
Namtumbo hadi Songea – Mbinga na Namtumbo – Tunduru unaendelea. Hivyo basi, kwa barabara ya “Mtwara Corridor” kazi iliyobaki ni kutoka Mbinga kwenda
Mbambabay ambayo tutaifanya wenyewe kama tulivyofanya kwa Mnazi Mmoja –
Nangurukuru na Somanga – Ndudu na Daraja la Umoja.
Ndugu Wananchi;
Ipo pia mipango
ya kuipanua na kuijenga upya bandari ya Mtwara ili iweze kuhudumia mahitaji ya utafutaji
na uchimbaji wa gesi baharini, kuhudumia na kuvifanyia matengenezo vyombo
vinavyotumika katika utafiti, uchimbaji na uendelezaji wa gesi. Pia iweze kuhudumia shughuli za kiuchumi
zitakazotokana na uchumi wa gesi pamoja na zilizopo sasa. Nilipozungumza na makampuni ya utafutaji gesi pale
Mtwara tarehe 25 Julai, 2011 waliomba nikubali bandari ya Mtwara iwe mahali pa
kuhudumia vyombo vyote vinavyofanya shughuli ya utafutaji na uchimbaji wa gesi
na mafuta katika pwani ya Afrika ya Bahari Kuu ya Hindi. Pia waliomba kuwa sehemu hiyo ya bandari iwe
bandari huru. Niliwakubalia bila ya
kusita na tayari eneo la hekta 110 zimeshatengwa
na kutangazwa rasmi kuwa bandari huru.
Vile vile waliomba wapewe sehemu ya bandari ya sasa kuendeshea shughuli
na eneo la kujenga kituo cha mitambo ya kuchakata gesi na kusafirisha nje.
Ndugu Wananchi;
Baada ya kuzungumza
na makampuni ya utafutaji gesi na mafuta na kuelezwa mahitaji yao nilibaini
kuwa bandari ya Mtwara inahitaji kupanuliwa na kujengwa upya. Bahati nzuri viongozi wa Mamlaka ya Bandari
walikuwepo na walinihakikishia kuwa watafanya hivyo.
Tayari eneo la
bandari limeongezwa kutoka hekta 70.68
hadi 2,693.68. Eneo la bandari huru limeshatengwa hivyo hivyo
na eneo la kampuni ya Dangote na makampuni ya gesi yaliyopo. Aidha, mchakato wa kupanua bandari iliyopo,
kujenga gati mpya na kuendelea na ujenzi hadi maeneo ya Msanga Mkuu ipo katika
hatua mbalimbali za matayarisho na utekelezaji.
Ndugu Wananchi;
Kwa
upande wa Mkoa wa Lindi mipango ya kupanua na kuijenga upya bandari ya Lindi
imefikia hatua nzuri. Naibu Waziri wa
Uchukuzi, Mhe. Dkt. Charles Tizeba alithibitisha hayo tarehe 1 Desemba, 2012
nilipotembelea bandari hiyo wakati wa ziara yangu ya Mkoa wa Lindi ya tarehe 1 mpaka
5 Desemba, 2012. Hali kadhalika mipango
ya kujenga bandari ya Kilwa iko mbioni.
Tena kwa upande wa Mkoa wa Lindi moja ya makampuni yaliyogundua gesi
baharini wameamua kujenga bandari na kituo cha kuchakata na kusarifisha gesi nje
ya mkoa huo kama ilivyo kwa Mtwara.
Naambiwa wametambua maeneo matatu, kilichobakia ni kuamua mojawapo ili ujenzi
uanze.
Ndugu Wananchi;
Nilipotoka bandari ya
Mtwara, siku ile nilitembelea Chuo cha VETA na kuzungumza na viongozi wa VETA
taifa na wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuhusu kuwa na mitaala ya
kutoa mafunzo mahsusi yanayohitajika na sekta ya gesi na mafuta. Nilisisitiza kwamba tuwapatie vijana wetu
mafunzo yatakayowawezsha kuajiriwa na makampuni ya gesi na yale yatakayokuwa
yanatoa huduma kwa makampuni hayo.
Nilisema tusipofanya hivyo, makampuni hayo yataajiri watu kutoka nje na
hatutakuwa na sababu ya kuwalaumu wala kulalamika.
Nafurahi kwamba
agizo langu hilo limefanyiwa kazi ipasavyo.
Hivi sasa katika chuo cha VETA Mtwara mafunzo hayo yanatolewa. Kampuni ya PetroBrass ya Brazil inaendesha
mafunzo ya sekta ya gesi kwa vijana 25 kutoka mkoani Mtwara. Aidha, chuo cha VETA kwa kushirikiana na
Kampuni ya Gesi ya Uingereza (British Gas) na Volunteers Service Overseas ya
Uingereza, kinatekeleza programu ya miaka mitatu iitwayo Enhancing Employerbility Through
Vocational Training. Programu
hii inalenga kutoa kozi zitakazowafanya
wahitimu kuweza kuajiriwa katika sekta ya gesi.
Programu hii ilifunguliwa na Makamu wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Mohamed
Gharib Bilal, tarehe 26 Novemba, 2012.
Ndugu Wananchi;
Chini ya
programu hii, walimu wa masomo yanayohusiana na gesi wanaongezewa ujuzi ili
waweze kufikia viwango vya kimataifa.
Vile vile, Wizara ya Nishati na Madini imetoa upendeleo maalum wa
kudhamini wanafunzi 50 kutoka mkoa
wa Mtwara kusoma chuoni hapo ambao tayari wameshahitimu mafunzo ya msingi ya
uunganishaji vyuma viwandani. Mchakato
wa kuwapata wanafunzi 50 kwa ajili
ya mafunzo kama hayo kutoka mkoa wa Lindi unaendelea. Nimeambiwa mpaka wameshawapata vijana 25 bado
25.
Hali
kadhalika, Wizara ya Nishati na Madini inadhamini wanafunzi 10 kupata mafunzo katika
Chuo Kikuu cha Dodoma ambako kozi za mafuta na gesi zinatolewa. Kipaumbele kwa udhamini huu unatolewa kwa
wanafunzi wa mikoa ya Mtwara na Lindi wenye sifa za kudahiliwa katika mafunzo
haya. Wamepatikana watatu. Wataalamu hawa na wengine wa fani mbalimbali
za gesi na mafuta watafundishwa kwa kiwango cha shahada ya kwanza na baadae
uzamili na uzamivu ili nchi yetu ijitosheleze kwa wataalamu wa sekta hii.
Kupanga
Mji wa Mtwara
Ndugu Wananchi;
Baada
ya kutembelea bandari ya Mtwara na Chuo cha VETA, nilikaa na kuzungumza na
viongozi wa Serikali na Manispaa ya Mtwara.
Katika mazungumzo yangu nao niliwasisitizia umuhimu wa kuwa na mpango
kabambe wa kuendeleza mji wa Mtwara – (Mtwara Masterplan) Mpango ambao utawezesha kujengwa mji mkubwa wa kisasa
unaokidhi mahitaji ya mji wa uchumi wa gesi.
Niliwataka wahakikishe kuwa kuna maeneo ya viwanda, biashara, makazi,
mahoteli, huduma za afya, elimu, mapumziko na burudani, viwanja vya michezo na
kadhalika. Kazi ya kutayarisha Masterplan hiyo imeanza na Manispaa ya
Mtwara inashirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi.
Kwa upande wa
uwekezaji nafahamu kuwa mpaka sasa makampuni 51 yameonyesha nia ya kuwekeza Mtwara katika viwanda, hoteli,
shughuli za uchukuzi na huduma hasa kwa sekta ya gesi. Wanachosubiri ni kutengewa maeneo ya kujenga,
waanze. Hivyo kukamilika mapema kwa Masterplan ya mji wa Mtwara kutasaidia
kuongeza kasi ya uwekezaji huu kufanyika.
Viwanda hivi vyote vitasaidia kuongeza ajira kwa vijana wa Mtwara na
Watanzania kwa jumla. Nimeambiwa kwa
mfano, wakati wa ujenzi wa kiwanda cha saruji watu zaidi ya 7,000 wataajiriwa.
Ndugu Wananchi;
Kabla
hata ya ugunduzi wa gesi iliyoko baharini, tulikuwa na mipango ya kutumia gesi
ya Msimbati (Mnazi Bay) kwa ajili ya kuzalisha umeme, kuzalisha mbolea na
kutumika katika kiwanda cha saruji. Kwa
upande wa umeme kulikuwa na mpango wa kujenga mtambo wa kuzalisha Megawati 300 kwa kushirikiana na
mwekezaji binafsi. Bahati mbaya wakati
wa matatizo ya kifedha ya dunia mwaka 2009 mwekezaji huyo akashindwa kupata
mkopo, hivyo mradi ukasimama kutekelezwa.
Haukufa wala haukuhamishiwa Dar es Salaam au Bagamoyo kama ambavyo
imekuwa inapotoshwa kwa makusudi. Mradi
huo bado upo, tena mpango wa sasa ni kujenga Megawati 600 zitumike Mtwara na zingine kuziingiza kwenye gridi ya
taifa kupitia Songea.
NduguWananchi;
Kwa upande wa
kiwanda cha mbolea, wawekezaji wengi wameshajitokeza tangu mwaka 2008 mpaka
sasa. Mchakato umefanyika wa kuchambua
wawekezaji wenye sifa na kutambuliwa.
Mambo mawili yamechelewesha utekelezaji kuanza. Jambo la kwanza ni wawekezaji na kampuni ya Artumas
iliyokuwa mbia na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (T.P.D.C) wakati ule,
kushindwa kukubaliana nao juu ya bei ya kuwauzia gesi. Wawekezaji walitaka bei ya gesi ipunguzwe,
lakini kampuni ya Artumas na T.P.D.C. hawakuwa tayari kupunguza zaidi ya kiasi
walichopunguza, ambacho wawekezaji bado waliona hailipi kwa kuzalisha mbolea.
Sababu ya pili ni matatizo ya kifedha
yaliyoikumba kampuni ya Artumas katika kipindi hicho. Kufuatia machafuko ya masoko ya fedha na
mdororo wa uchumi wa dunia mwaka 2008/2009 kampuni ya Artumas iliathirika na
kulazimika kuuza hisa zake kwa wawekezaji wengine. Katika kipindi hicho ilichopitia kampuni,
mazungumzo na uwekezaji wa kiwanda cha mbolea hayakuweza kupewa kipaumbele. Mtazamo wa sasa wa wabia wapya na T.P.D.C. ni
kuwa wao wenyewe sasa wawekeze katika ujenzi wa kiwanda cha mbolea. Serikali
imekubali rai yao hiyo na wanaendelea na matayarisho.
Ndugu Wananchi;
Kwa
upande wa kiwanda cha Saruji kitakachojengwa na kampuni ya Dangote
ucheleweshaji ulikuwa kwa sababu mbili.
Kwanza, kampuni ya Dangote iliomba eneo zaidi ya ililokuwa imeomba na
kupewa. Hoja yao ilikuwa kwamba eneo la
ziada walilokuwa wanaliomba ndilo lenye malighafi nyingi na bora kwa
utengenezaji wa saruji. Hivyo, waliamua
kusubiri mpaka watakapopewa eneo hilo.
Bahati mbaya
eneo hilo lilikuwa linamilikiwa na mtu mwingine na alikuwa na hati miliki
nalo. Halmashauri ya Mtwara iliomba
Serikali eneo hilo litwaliwe na baadaye ipewe kampuni ya Dangote. Serikali
ilikubali. Hata hivyo, mchakato
ulichukua muda na hata pale ulipokamilika mwenye eneo aliupinga uamuzi wa
Serikali Mahakamani. Kesi ilichukua muda
kusikilizwa na kumalizika. Bahati nzuri
Serikali ikashinda na mara baada ya uamuzi wa Mahakama ndipo kampuni ya Dangote
ikamilikishwa eneo hilo.
Kampuni nayo
ilichukua muda kuanza. Hivi sasa, timu
yake ipo kwenye eneo na mradi uko tayari kuanza kutekelezwa. Niliambiwa kuwa katika magari yaliyopigwa
mawe katika fujo za Mtwara ni pamoja na lile la mradi huu. Huo ndiyo ukweli kuhusu ujenzi wa kiwanda cha
saruji cha Dangote. Madai kuwa kiwanda
hicho kimehamishiwa Bagamoyo si ya kweli.
Ni uzushi wa makusudi wa watu
wenye nia mbaya na Serikali. Huwezi
kudai kuwa mtetezi wa wananchi wa Mtwara kwa hoja za uongo na kufanya upotoshaji
wa makusudi kabisa.
Ndugu Wananchi;
Ujenzi
wa bomba la gesi ndiyo uliozua mzozo wote huu.
Zilijengwa hisia kuwa gesi yote inapelekwa Dar es Salaam na kwamba Mtwara
itakosa gesi na maendeleo yatayotokana na gesi hiyo. Na, wengine wakasema gesi inapalekwa Bagamoyo
ili kuzidisha chumvi na kupandikiza chuki kwa wananchi dhidi ya Serikali kwamba
Rais anapeleka gesi kwao. Kwanza, Kinyerezi iko Ilala na siyo Bagamoyo. Pili, ukweli ni kwamba pale Mtwara kuna gesi
nyingi ya kutosheleza mahitaji ya Mtwara, Lindi na Dar es Salaam na kubaki. Gesi itakayoletwa Dar es Salaam ni asilimia 16 tu ya gesi yote iliyoko Mtwara
kwa miaka ishirini ijayo. Hivyo asilimia 84 ya gesi itabaki Mtwara kwa
ajili ya kuuzwa nje ya nchi na kupelekwa kwingineko nchini.
Kwa
sababu hiyo, ndugu zetu wa Mtwara hawana sababu ya kuwa na wasiwasi. Ipo gesi
ya kutosha kwa mahitaji ya sasa na ya miaka mingi ijayo. Viwanda vinavyotumia gesi kama mali ghafi na
vile vinavyohitaji gesi kama nishati vyote vitapata gesi ya kutosha. Kwa upande wa uzalishaji umeme hali kadhalika
ipo gesi ya kutosha kuzalisha umeme mwingi zaidi. Hivi sasa tunacho kituo kinachozalisha umeme
wa megawati 15 unaotumika Mtwara,
Lindi, Tandahimba, Newala, Masasi, Nachingwea, Ruangwa, na Mtama. Bado umeme
huo hautumiki wote hivi sasa.
Ndugu Wananchi;
Nayaeleza
yote
haya kuwathibitishia wananchi wa Mtwara kuwa tunawathamini sana na
kuwajali. Mimi nitakuwa mtu wa mwisho kuwapuuza
na kuwatupa mkono wananchi wa Mikoa ya Kusini.
Aidha, sitakuwa tayari kuwaruhusu watu au mtu ye yote Serikalini
kuwapuuza wananchi wa Mikoa ya Kusini au mkoa wo wote hapa nchini. Hiyo
haitakuwa sawa. Nilishasema siku za nyuma na napenda kurudia
tena leo kuwa kwangu mimi hakuna mkoa ulio bora kuliko mwingine. Ni
kutokana na msimamo wangu huo ndiyo maana
tumeelekeza nguvu na rasilimali nyingi za Serikali katika mikoa
iliyokuwa inadaiwa kuwa imesahauliwa. Kazi ya ujenzi wa barabara za
lami iliyofanyika
na inayoendelea kufanyika katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Rukwa,
Kigoma
na Kagera inajieleza yenyewe. Mipango ya kuboresha Kiwanja cha Ndege cha
Mtwara
kufikia hadhi ya kimataifa na uboreshaji wa viwanja vya ndege vya Lindi
na
Kilwa ni ushahidi mwingine kati ya mambo mengi tunayoweza kuyataja.
Ndugu Wananchi;
Haya
niliyoyasema ni sehemu ndogo tu ya yale yaliyofafanuliwa na kuelezwa kwa kina
na Mawaziri na Wakuu wa Idara husika za
Serikali na Mashirika ya Umma pale Mtwara
katika mkutano wa Waziri Mkuu na viongozi wa Serikali, dini, vyama vya siasa na
wazee wa Mkoa wa Mtwara tarehe 29 Januari, 2013.
Ndugu Wananchi;
Napenda
kutumia nafasi hii kutoa pongezi nyingi kwa Waziri Mkuu, Mheshimiwa Mizengo
Pinda, kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanya kule Mtwara. Uvumilivu wake, usikivu wake na utulivu wake
vimesaidia sana kulivusha taifa katika moja ya mitihani mikubwa ambayo ingeikuta
nchi yetu tangu Uhuru. Nawapongeza Mawaziri
na Wakuu wa Mashirika ya Umma na Idara za Serikali kwa mchango wao muhimu
walioutoa, uliosaidia kufafanua masuala ambayo yalikuwa hayaeleweki
vizuri. Kwa wao nawasisitiza na
kuwakumbusha wajibu wao wa kuelimisha jamii kuhusu shughuli wazifanyazo. Wakifanya hivyo mara kwa mara migongano
haitakuwepo na wapotoshaji hawatapata nafasi.
Ndugu Wananchi;
Nitakuwa
mwizi wa fadhila kama sitawashukuru viongozi wa Serikali, vyama vya siasa, madhehebu
ya dini, viongozi wa jamii, wazee, wana-Mtwara na makundi mbalimbali ya jamii, kwa
muda waliotumia kuzungumza na Waziri Mkuu na kuwasikiliza wasaidizi wake
wakifafanua masuala mbalimbali.
Uvumilivu wao na uelewa wao ndivyo vilivyosaidia kurejesha hali kuwa ya
kawaida. Nawaomba nao sasa, wote kwa
pamoja washirikiane na Serikali kuelimisha umma kuhusu ukweli wa mambo. Pia watumie nafasi hiyo kutahadharisha jamii na
kuwataka watu kuwa waangalifu na kupima maneno wanayoambiwa na watu. Wajiepushe na maneno au vitendo vinavyofarakanisha,
kuchonganisha na kupandikiza chuki dhidi ya watu au Serikali. Waambieni kuwa
ghasia hukimbiza wawekezaji kwani wakipata hofu kuwa hali ya amani na usalama
ni ya mashaka, watatoka kwenda kuwekeza kwingine. Vyema iwe hapa hapa nchini, lakini wanaweza
kwenda nchi nyingine na sisi kupoteza kabisa.
Ndugu Wananchi;
Nawapa
pole wananchi wa Mtwara na Masasi kwa usumbufu walioupata kutokana na
ghasia
zilizofanywa. Nawapa pole waliofiwa na
kujeruhiwa. Nawapa pole waliopoteza au
kuharibiwa mali zao. Kwa kweli inasikitisha
na kufadhaisha kuona watu wanafanya vitendo vya kuua, kuchoma moto
nyumba za
watu na majengo ya Serikali pamoja na , kuharibu na kuiba mali za watu.
Huu ni uhalifu ambao hauna maelezo na haukubaliki. Tunaviachia vyombo
husika vya dola na sheria kutimiza
wajibu wao. Kwa waliohusika iwe fundisho
kwao na kwa wengineo kutokubali kutumika kwa maslahi ya watu wengine
siku
zijazo. Sasa wameachwa pekee yao wakati
wenzao wako huru na kufaidi maisha
Ndugu Wananchi;
Hili sakata la
bomba la gesi limefika mahali pazuri.
Yaliyopita si ndwele tugange yajayo.
Mungu
Ibariki Afrika!
Mungu
Ibariki Tanzania!
Asanteni
Sana kwa Kunisikiliza!
Subscribe to:
Posts (Atom)