Karibu katika blog yetu

Wednesday, January 16, 2013

MABWEPANDE: ELIMU BADO NI CHANGAMOTO

Picha kwa hisani.ya One Mocke Blog.

Upungufu wa walimu umeelezwa kuwa ni moja ya sababu zinazochangia matokeo yasiyoridhisha katika shule ya msingi Mabwepande iliyoko katika manispaa ya Kinondoni

Mwalimu mkuu wa shule hiyo  Davis Mkaruka amesema idadi ya walimu waliopo shuleni hapo haitoshelezi mahitaji halisi ya wanafunzi
Amesema shule hiyo ina jumla ya walimu 15 huku ikiwa na wanafunzi zaidi ya elfu moja

Mwalimu mkuu huyo amesema katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba mwaka jana wanafunzi 30 kati ya 94 ndio waliofaulu mtihani,matokeo ambayo amesema bado hayaridhishi

Ameiomba idara ya elimu katika manispaa ya Kinondoni kuongeza idadi ya walimu pamoja na kutoa mafunzo ya mara kwa mara ili walimu waweze kumudu mabadiliko ya mitaala

No comments:

Post a Comment