Karibu katika blog yetu

Thursday, July 25, 2013

MPOTO ALIA NA BONGO FLAVOUR!




Mwanamuziki na mtunzi wa mashairi mahiri nchini Mrisho Mpoto amesema wasanii wengi wa muziki wa kizazi kipya (Bongo Flavour) ni wafanyabiashara zaidi hivyo wanashindwa kutetea na kuitambulisha jamii ama hadhira inayowazunguka.

Mpoto amesema hayo na Mlimani TV wakati wa kongamano la Muziki wa Afrika lililoanza hii leo
 (25/07/2013) idara ya sanaa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Msanii huyo anayejulikana kwa jina la "Mjomba" amesema kuwa tofauti na nchi kama Senegal ambayo ina Youssou n'dour na Marekani, Michael Jackson, Tanzania mpaka sasa hakuna msanii ambaye anaweza akawa kitambulisho cha sanaa ya muziki nchini.


Katika hatua nyingine, Mpoto amesema vyombo vya habari vinakabiliwa na changamoto kubwa ya kuutangaza muziki wa Tanzania ndani na nje ya nchi.

Kongamano la Muziki wa Afrika linaloendeshwa na idara ya sanaa ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam linaendelea na linatarajia kufikia kilele chake siku ya jumamosi kwa wahadhiri, nguli mbalimbali wa muziki kutoka nchi mbalimbali duniani kuwasilisha mada kuhusiana na muziki.

Maxmillian John Ngube, Hawa, Shumu, Emmanuel Kihwelu

KAMERA YETU

Mkulima katika kijiji cha Chiwerere mkoani Lindi akipiga piga mahindi baada ya kuvuna

Binti akiweka mahindi sehemu nzuri baada ya kuyavuna katika kijiji cha Chiwerere Lindi

Daladala kutoka kijiji cha Kijiweni mpaka Lindi

Mvuvi katika kijiji cha Kijiweni, Lindi

Kijiji cha Tchezema kilichopo Mvomero mkoano Morogoro

Sunday, July 14, 2013

TBS: HATUWEZI KUBAINI SIMU FEKI

Shirika la viwango nchini TBS limesema kuwa kwa sasa halina teknolojia inayowawezesha wataalamu wake kubaini simu zisizo na viwango ama feki.

Afisa uhusiano wa TBS, Bi Roida Andusanile akiongea na Mlimani TV amewataka wananchi kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho shirika lake linajipanga kuhakikisha inapata teknolojia hiyo ili kudhibiti uingizwaji wa simu hizo ambao umekuwa ukiongezeka kwa kasi katika maeoneo mengi nchini hususa katika jiji la Dar es Salaam.

Anuary Mkama.