Karibu katika blog yetu

Monday, January 7, 2013

CUF YAWASILISHA MAONI YAKE KWA TUME YA KATIBA


Chama cha wananchi Tanzania CUF kimeshauri kwamba kuna umuhimu wa serikali TATU katika katiba mpya itakayoundwa ili kuondoa migongano na kero za Muungano.

Akiongea mara baada ya kutoa maoni yao kwa tume ya katiba,Mwenyekiti wa CUF Profesa Ibrahim Haruna Lipumba amesema kuwa amesema muundo wa serikali tatu utalifaa taifa la Tanzania,amezitaja serikali hizo kuwa ni pamoja na serikali ya Tanganyika,Zanzibar na Muungano.

Profesa Lipumba amesema kuwa kumekuwepo na Malalamiko hasa kutoka upande wa Zanzibar kuwa serikali ya Tanganyika imemezwa nay a Muungano kutokana na muundo wa sasa.

Aidha katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo amesema suala la rasilimali za nchi hiii zinatakiwa ziwekwe kikatiba ili kila mwananchi aweze kufaidi matunda ya Uhuru wa nchi hii.

Masuala mengine yaliyopendekezwa na chama hicho kwa tume ya katiba ni pamoja na suala la uteuzi wa viongozi, usawa wa kijinsia,maadili ya viongozi na kuwepo kwa tume huru ya uchaguzi ili kutoa fursa sawa ya kidemokrasa katika  siasa.

No comments:

Post a Comment