Karibu katika blog yetu

Thursday, November 8, 2012

PROF. KILLIAN AWATAKA WANASISA NCHINI KUWA NA ITIKADI INAYOELEWEKA

MHADHIRI mwandamizi wa masuala ya uongozi na siasa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye pia ni mchambuzi wa masuala ya siasa duniani Professor Bernadetta Killian amewataka wanasiasa kuhakikisha wanakuwa na sera na itakadi zinazoelewaka wakati wakiwa wanajinadi katika majukwaa ili wapigiwe kura kushika nyadhifa mbalimbali.

Prof. Bernadeta Killian
Prof. Killian amesema hayo wakati akiongea na Mlimani TV na kuongeza kuwa Rais mteule wa Marekani Barack Obama ameshinda kwa mara nyingine tena kutokana na kuwa na sera na mlengo unaoelewaka kiasi cha kuweza kuwashawishi vijana na wanawake wengi kumpigia kura na hatimaye kumshinda mpinzani wake wa chama cha Republican Mitt Romney.

No comments:

Post a Comment