Karibu katika blog yetu

Sunday, June 16, 2013

Sabri Lamouchi aikubali Stars!


Thomas Ulimwengu



Nadir Haroub
Sabri Lamouchi


Juma Kaseja akijitahidi kuokoa mpira wa tuta uliopigwa na Yahya Toure


Thomas Ulimwengu



Juma Kaseja

Kim Poulsen akimlalamikia kamisaa kuhusiana na penalty

Kim Poulsen akiwalalamikia waaamuzi baada ya mapumziko
Licha ya timu yake kuibuka na ushindi mnono dhidi ya Tanzania, Taifa Stars, kocha mkuu wa Ivory Coast Sabri Lamouchi amesifu kiwango cha kilichooneshwa na Stars.
kocha huyo kijana amesema kuwa amefurahishwa zaidi na uwezo wa washambuliaji wa Stars ambao walikuwa wanaliandama lango la timu yake kila mara.

Nao wachezaji wa Stars, Juma Kaseja, Frank Domayo, Mbwana Samatta, Nadir Haroub wameitaka serikali na TFF kuendelea kuipa maandalizi mazuri timu ya taifa kwa mashindano mengine yanayokuja.
                                        
Mbwana Samatta

Akiongea zaidi Mbwana Samatta anayecheza katika klabu ya TP Mazembe ya DRC amesema kuwa nafasi anayocheza kwa sasa kama winga wa pembeni imekuwa ngumu kwake kutokana na kulazimika kurudi nyuma kusaidia safu ya ulinzi tofauti na anapokuwa katika klabu ya TP Mazembe, lakini amesema anafurahia kucheza kwani ni nafasi aliyokuwa anacheza awali lakini pia Kim Poulsen ndiyo nafasi anayopenda zaidi kumuona akicheza.


kutokana na matokeo hayo sasa, Ivory Coast imeungana na Ethiopia, Misri na Tunisia kutinga katika hatua ya mtoano ya kutafuta wawakilishi watano pekee ambao wataliwakilisha bara hili katika fainali za dunia za mwaka 2014 nchini Brazil.