Karibu katika blog yetu

Monday, April 8, 2013

TABORA NA MASOMO YA JIONI KWA KIDATO CHA NNE

Mkoa wa Tabora umeamua kutoa nafasi za masomo ya jioni kwa wanafunzi waliofeli kidato cha nne hivi karibuni ili kuwapa nafasi waweze kusawazisha makosa yao na hatimaye waendelee na masomo ya ngazi ya juu.
Afisa elimu wa mkoa huo Midamo Paul Makungu amesema kuwa ofisi yake imeshakubaliana na walimu wa shule za sekondari kuanzisha masomo hayo kwa wanafunzi watakaopenda.

No comments:

Post a Comment