Wachezaji wa timu ya taifa ya Nigeria wamepokea kiasi cha
dola 30,000 kila mmoja kutoka shirikisho la soka la nchi hiyo kwa kufanikiwa
kutinga katika hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la mataifa ya Afrika.
Fedha hizo zimetolewa na shirikisho la soka la Nigeria NFF
ili kuwapa motisha wachezaji kushinda katika mchezo wake unaofuata dhidi ya
Ivory Coast unaotarajiwa kuchezwa wikend hii.
Toka ianze michuano ya kombe la mataifa ya Afrika Nigeria
imeshiriki michuano hiyo mara 17 na imefanikiwa kusonga mbele mara 15.
Wakati Nigeria wakipokea kiasi hicho cha fedha, Ghana
wamepokea dola 5000 kila mmoja kwa kuingia hatua hiyo ya robo fainali.
No comments:
Post a Comment