Kocha mkuu wa klabu ya Arsenal, Arsen Wenger amekiri kuwa
safu yake ya ulinzi imekuwa ikilega lega na kuruhusu magoli ambayo yamekuwa
yakiigharimu timu hiyo katika michezo yake ya ligi kuu na ile ya klabu bingwa
ya Afrika.
Wenger amesema kuwa kikosi chake kimekuwa kikionesha soka
safi lakini upande wa safu ya ulinzi umekuwa haupo imara na kuruhusu magoli
hivyo anaamini usajili wa mlinzi wa kushoto raia wa Uhispania Nacho Monreal
unaweza ukaimalisha safu yake ya ulinzi.
Katika hatua nyingine Wenger amesema ataendelea kumtumia
mlinzi wake wa kushoto kutoka Brazil Adrea Santos na anaamini ndiye ataziba pengo la Gibbs
katika mchezo wa klabu bingwa ulaya dhidi ya Bayern Munich.
No comments:
Post a Comment