Karibu katika blog yetu

Monday, March 25, 2013

Stars yamuweka matatani Taoussi

Majaliwa ya kocha mkuu wa Morocco Rachid Taoussi kuendelea kuifundisha timu ya taifa ya nchi hiyo yapo mashakani baada ya wadau wa soka wa Morocco kutaka kocha huyo ajiuzuru kutokana na kufungwa goli 3-1 na Tanzania katika mchezo wa kuwania kucheza kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

Wadau hao wa soka nchini humo wamesema kuwa kocha huyo ameshindwa kuiletea timu yao mafanikio lakini wameponda pia kitendo chake cha kufanya mabadiliko makubwa katika kikosi kilichocheza katika michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika na kile kilichopata kipigo cha aibu kutoka kwa Tanzania.

Morocco sasa inahitaji miujiza ili isonge mbele katika hatua nyingine ya kuwania nafasi ya kucheza fainali zijazo za dunia nchini Brazil.


No comments:

Post a Comment