Karibu katika blog yetu

Tuesday, April 9, 2013

Kigoma yakabiliwa na uhaba wa walimu wa sayansi.

Imeelezwa kuwa mkoa wa Kigoma unakabiliwa na upungufu mkubwa wa walimu wa somo la sayansi hali ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi wa kidato cha nne na sita kushindwa kufanya vizuri katika mitihani yao ya taifa.

kauli hiyo imetolewa na Afisa elimu msaidizi wa Kigoma bwana Venance Babukege wakati akizungumzia maendeleo ya elimu ya mkoa huo.

Bwana Babukege amesema idadi wa walimu wa masomo ya sanaa inaridhisha huku upande wa sayansi hali ni mbaya zaidi hivyo kusababisha wanafunzi wengi wasichague michepuo ya masomo hayo huku wale waliochagua nao wakipata matokeo ambayo hayaridhishi.

kwa upande wa walimu wanaofundisha masomo ya sayansi, babukege amesema wamekuwa wakiomba uhamisho pindi wanapopangiwa kigoma kutokana na kukosekanika nyenzo za kufundishia kwa vitendo.

katika mipango ya kujipanga kuhakikisha kiwango cha ufaulu kinaongezeka hususa kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka huu, Babukege amesema kuwa hivi sasa kitengo chake kinatembelea katika shule zote za sekondari za mkoa kuzungumza na walimu ili kupata njia ambazo zitasaidia kuinua kiwango cha ufaulu.

Anuary- Kigoma.

No comments:

Post a Comment