Karibu katika blog yetu

Saturday, November 24, 2012

HAYATOU APONGEZA JITIHADA ZA CECAFA

Rais wa CAF Issa Hayatou.
Rais wa Shirikisho la soka Afrika, CAF, Issa Hayatou amesifu jitihada za baraza la michezo la Afrika mashariki CECAFA kwa jitihada zake za kuhakikisha mchezo wa kandanda unakua katika ukanda huu.
Hayatou amesema kuwa anaheshimu sana jitihada za baraza hili na ndio maana alikubali mwaliko wa kushuhudia ufunguzi wa fainali za michuano hii licha ya kuwa na shughuli nyingine muhimu.
Ameyataka mashirikisho mengine kuiga mfano wa CECAFA katika kuhakikisha maendeleo yanakuza maendeleo ya soka katika kanda zao.


No comments:

Post a Comment