Karibu katika blog yetu

Thursday, November 8, 2012

HU JINTAO AAHIDI MABADILIKO YA KISIASA NCHINI CHINA

WAKATI serikali ya Jamuhuri ya watu wa China ikiwa katika kipindi cha mabadiliko ya uongozi wa juu wa nchi hiyo, Rais anayemaliza muda wake Hu Jintao ameahidi mabadiliko ya mfumo wa kisiasa ambao utatoa fursa zaidi kwa vijana wa nchi hiyo kuweza kushika nafasi za juu katika dola ya nchi hiyo iliyopiga hatua kubwa kiuchumi kuliko nchi yoyote kwa sasa duniani.

Mfumo wa kisiasa wa China ambao ni wa chama cha Kikomunisti umekuwa ukionekana kuwabana zaidi vijana wa nchi hiyo kuchagua na kushika nafasi za utawala.

Katika hatua nyingine Hu Jintao amekiri kuwa suala la rushwa litakimaliza chama hicho endapo kama wanachama na viongozi wa chama hicho hawataondokana na tatizo hilo. 

No comments:

Post a Comment